

Lugha Nyingine
如何让超宽带(UWB)信号测试变得简单易行?
Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania ameweka jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa Eneo Maalum la Kiviwanda la Kwala, lililopo wilayani Kibaha mkoani Pwani.
Eneo hilo maalum ni mradi wa ubia wa kampuni sita, likiwa linajengwa kwenye eneo lenye ukubwa wa ekari 2,500 na likitarajiwa kuwa na viwanda zaidi ya 200.
Mkuu wa eneo hilo maalum Bw. Janson Huang amesema mradi huo unalenga kuifanyia mageuzi Tanzania kuwa kitovu kinachoongoza kwa biashara, uzalishaji wa kiviwanda na uvumbuzi wa nishati safi.
Bw. Huang amesema tayari kuna viwanda 12, saba kati ya hivyo vinafanya kazi na vitano vinaendelea kujengwa, na kwamba kwa sasa eneo hilo maalum limeajiri zaidi ya watanzania 1,000, idadi ambayo inatarajiwa kufikia 5,000 ifikapo mwishoni mwa mwaka kesho.
Miongoni mwa malengo ya siku za baadaye ni eneo hilo maalum ni kuunga mkono utengenezaji wa betri za magari ya umeme, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kimataifa za kupunguza uzalishaji wa kaboni ifikapo 2050.
Miujiza ya Wanyamapori: Kutoka Mbuga Tambarare za Afrika hadi Uwanda wa Juu wa Qinghai -Tibet, China
Mandhari ya Kipekee ya Karst katika Mkoa wa Guizhou yavutia watalii
Tamasha la kimataifa la densi lafunguliwa katika Mkoa wa Xinjiang, China likiwa na maonyesho 52
Wakulima wa China wawa na pilikapilika za uzalishaji wa kilimo katika kipindi cha Dashu
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma