

Lugha Nyingine
榻榻米床垫什么材质的好
Rais wa Kenya William Ruto amesaini Mswada wa Mgongano wa Maslahi kuwa sheria jana Alhamisi ili kusaidia kuimarisha vita dhidi ya ufisadi nchini.
Kwenye taarifa iliyotolewa mjini Nairobi baada ya kusainiwa mswada huo, Ruto amesema sheria hiyo mpya inayobatilisha Sheria ya Maadili ya Maafisa wa Umma, inaleta muundo wa kina wa kudhibiti migongano ya kimaslahi serikalini ili kudhibiti matumizi mabaya ya mamlaka ya maafisa wa umma, kuhakikisha rasilimali za umma zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.
Aidha Ruto amesisitiza kuwa sheria hiyo mpya inaweka sheria wazi ili kuhakikisha maafisa wa umma wanahudumu kwa uadilifu, uwazi na uwajibikaji.
Amebainisha kuwa sheria hiyo mpya pia inawapa Wakenya fursa ya kuwawajibisha maafisa wa umma katika kutekeleza mamlaka yao.
Sheria hiyo inaipa mamlaka Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) ya kusimamia utekelezwaji wake, na chombo hicho cha kupambana na ufisadi kitashughulikia masuala yanayohusiana na kutangaza mali kwa maafisa wote wa umma, si tu kwa Watendaji Wakuu bali pia hata katika Bunge na Mahakama.
Mandhari ya Kipekee ya Karst katika Mkoa wa Guizhou yavutia watalii
Tamasha la kimataifa la densi lafunguliwa katika Mkoa wa Xinjiang, China likiwa na maonyesho 52
Wakulima wa China wawa na pilikapilika za uzalishaji wa kilimo katika kipindi cha Dashu
Maliasili nyingi za chumvi zaongeza mapato ya wanakijiji katika Wilaya ya Gegye, Xizang, China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma